Thursday, November 29, 2012

Ligi ya NBA kuoneshwa ATN live

Na Silas Nicodem.
Kituo cha Televisheni ya Agape kwa kushirikiana na Agape Association wanatarajia kurusha mechi za mpira wa kikapu za nchini Marekani.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, afisa mahusiano wa ATN/TING, Brian Urassa amesema kuwa lengo la kurusha matangazo hayo ni kuleta hamasa kwa watanzania wenye vipaji vya mpira wa kikapu.

 “Tanzania tunawachezaji wawili tu nao ni Martin Ndunguru na Hashim Thabiti ambao ndio maarufu wanaocheza mpira wa kikapu nchini Msarekani, je wengine watahamashishwaje, hivyo ni bora tuanziashe maonesho hayo na vipaji vingine vitajitokeza” alisema Urassa.

Urassa aliongeza kuwa mara nyingi mpira wa miguu ndio umekuwa na mashabiki wengi kuliko mpira wa kikapu hivyo basi kwa kufanya hivi tutaweza kuongeza idadi ya mashabiki wa pmira wa kikapu, na kuweza kuhamasisha timi za kikapu nchini.

Akielezea ratiba za mechi hizo katika ATN zitakazoanza kuoneshwa manamo juma pili ya tarehe 1, Desemba mwaka huu, Urassa amesema mechi zitakuwa zikioneshwa kila siku ya jumapili, saa 9 hadi saa 10 alfajiri na kurudiwa kila jumapili saa 8:30 mchana,na mechi itakayokuwa ya kwnza kuoneshwa ni kati ya Brooklyn dhidi ya Miami.

No comments:

Post a Comment